Kituo Kipya cha Msaada wa Majanga Chafunguliwa katika Jiji la St. Louis: Masaa katika Vituo vyote vya Msaada wa Majanga Yatabadilika Jumatatu

Release Date Release Number
012
Release Date:
Septemba 9, 2022

Kituo kipya cha Msaada wa Majanga cha FEMA kitafunguliwa Jumamosi, Septemba 10, katika Jiji la St. Louis ili kutoa usaidizi wa ana kwa ana kwa watu walioathiriwa moja kwa moja na mafuriko ya Julai 25—28 na dhoruba kali.

Wataalamu wa Misaada kutoka FEMA na Usimamizi wa Biashara Ndogo za Marekani watatoa taarifa kuhusu huduma zinazopatikana, kueleza mipango ya usaidizi na kuwasaidia walionusurika kukamilisha au kuangalia hali ya maombi yao.

Vituo vya msaada wa majanga vinapatikana katika:

Kituo cha Salvation Army Temple

2740 Arsenal St

St. Louis, MO 63118

(Karibu na kona ya Arsenal na California)

Masaa ya jumamosi: saa mbili asubuhi (8 a.m.) – saa kumi na moja jioni (5 p.m.)

Kuanzia Jumatatu, Septemba 12, masaa mapya za vituo vyote vya msaada itakuwa:

Jumatatu – Ijumaa, saa mbili asubuhi (8 a.m.) – saa kumi na mbili jioni (6 p.m).

Jumamosi, saa mbili asubuhi (8 a.m.) – saa kumi na moja jioni (5 p.m.)

Inafungwa Jumapili

Vituo vingine vya msaada vimefunguliwa katika maeneo haya:

JIJI LA ST. LOUIS

Chuo cha Ranken Technical

Kituo cha Teknolojia cha Mary Ann Lee

1313 N. Newstead Ave.

St. Louis, MO 63113

(Kwenye kona ya Newstead na Page)

KAUNTI YA ST. LOUIS

Kituo cha Urban League Empowerment

9420 W. Florissant Ave.

Ferguson, MO 63136

Kituo cha University City Recreation

Centennial Commons

7210 Olive Blvd.

University City, MO 63130

Kituo Hazelwood Civic

8969 Dunn Road

Hazelwood, MO 63042

KAUNTI YA ST. CHARLES

Kituo cha Manispaa ya O’Fallon

100 N. Main St.

O’Fallon, MO 63366

(Kiingilio cha Kusini-mashariki)

Bodi ya Rasilimali za Ulemavu Unaoendelea – Jengo la DDRB

1025 Country Club Road

St. Charles, MO 63303

(I-70 karibu na njia ya kutoka Zumbehl)

Eneo la DDRB litafungwa kabisa Jumatano, Septemba 14, saa kumi na mbili jioni (6pm).

Hakuna miadi inahitajika kutembelea Kituo cha Msaada wa Majanga. Wanaokuja bila miadi wanakaribishwa

Watu walioathiriwa moja kwa moja na mafuriko katika Jiji la St. Louis, Kaunti ya St. Louis na Kaunti ya St. Charles wanaweza kutembelea kituo chochote cha msaada.

Ikiwa unahitaji msaada kutuma maombi, FEMA inaweza kukusaidia katika Kituo cha Msaada wa Majanga.

Tuma ombi na FEMA mtandaoni kwenye DisasterAssistance.gov au piga simu 800-621-FEMA (3362).

FEMA inaweza kutoa pesa za ruzuku ya Usaidizi wa Mtu Binafsi ambazo si lazima zilipwe kwa:

  • Msaada wa Kodi ya Nyumba ikiwa unahitaji kuhama kwa sababu ya uharibifu wa mafuriko
  • Mali ya kibinafsi ambayo iliharibika au kuharibiwa na mafuriko
  • Kurudishiwa Malipo ya Mahali pa kulala ikiwa ulilazimika kukaa katika hoteli kwa muda
  • Marekebisho ya Msingi ya Nyumba kwa wamiliki wa nyumba ambao makazi yao ya msingi yaliharibiwa na mafuriko
  • Mahitaji Mengine Muhimu yaliyosababishwa na mafuriko ya hivi karibuni

Mbali na msaada ulioorodheshwa, tafadhali kumbuka yafuatayo:

  • Ombi moja tu kwa kila familia
  • FEMA hailipii chakula kilichopotea au kuharibika
  • Kisheria, Fema hairuhusiwi kulipia tena malipo ya bima au usaidizi uliotolewa na vyanzo vingine

Wamiliki wa Nyumba na Wapangaji: Baada ya kutuma maombi na FEMA Ikiwa umetumwa kwa SBA kwa ajili ya mkopo wa majanga, tafadhali wasilisha ombi. Kuwasilisha ombi la SBA hukuwezesha kuzingatiwa kwa ajili ya ruzuku za ziada ikiwa utanyimwa mkopo wa SBA.

Ikiwa unastahili kupata mkopo, utakuwa na rasilimali hiyo ikiwa utachagua kuikubali.

Usaidizi wa ombi lako la SBA unapatikana katika Vituo vyovyote vya Msaada wa Majanga.                              

Kwa masasisho, tufuate kwenye Twitter @MOSEMA na @FEMARegion7.

Pata habari mpya kwa Recovery.MO.gov na FEMA.gov/disaster/4665.

Usaidizi wa majanga unapatikana bila kuzingatia rangi, dini, utaifa, jinsia, umri, ulemavu, ujuzi wa Kiingereza au hali ya kiuchumi.

Tags:
Ilisasishwa mara ya mwisho